SHULE BORA YAWAJENGEA UWEZO WALIMU WA HISABATI JIJINI TANGA.
Автор: Tangajiji tv
Загружено: 2025-12-12
Просмотров: 16
Halmashauri ya jiji la Tanga kupitia mradi wa shule bora imeendelea kutoa mafunzo kwa walimu 75 wanaofundisha masomo ya hisabati katika jiji la Tanga.
Akielezea matumaini mafunzo hayo kwa walimu Afisa elimu Jiji la Tanga Shomari Bane amesema kwa sasa walimu wanapatiwa mafunzo ya stadi tatu za KKK , English na Hisabati zitakazotumika kuanzia darasa la kwanza kwa mtaala ulioboreshwa.
Mwalimu Bane amesema some la hisabati katika jiji la Tanga halifanyi vizuri katika ufaulu ndiyo sababu ya kuleta mafunzo hayo yatakayosaidia kukuza usomaji na ufundishaji kwa mbinu mpya na za kisasa.
Pia Bane ameelezea umuhimu wa walimu kupata mafunzo mbalimbali ya kuongezewa ujuzi wa kufundisha kwani kufanya hivyo kunaongeza umahiri katika kazi zao.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: