Популярное

Музыка Кино и Анимация Автомобили Животные Спорт Путешествия Игры Юмор

Интересные видео

2025 Сериалы Трейлеры Новости Как сделать Видеоуроки Diy своими руками

Топ запросов

смотреть а4 schoolboy runaway турецкий сериал смотреть мультфильмы эдисон
dTub
Скачать

SERIKALI YAAHIDI SHERIA RAFIKI KWA WAWEKEZAJI KUFANIKISHA DIRA 2050

Автор: Mtanzania Digital

Загружено: 2025-10-16

Просмотров: 50

Описание:

Kibaha, Pwani. Serikali imeeleza dhamira yake ya kutengeneza sheria rafiki za uwekezaji zitakazoiwezesha kufikia uchumi wa kati wa juu kama ilivyobainishwa kwenye Dira 2050.

Moja ya shabaha za Dira 2050 ni kuchochea ukuaji wa Pato la Taifa kutoka yapata $80 billioni ya sasa mpaka $1trilioni ifikapo mwaka 2050.

Kufikia lengo hilo, serikali imesema ni lazima iendelea kutengeneza mazingira mazuri ya biashara yatakayowezesha taasisi za umma kufanya vizuri kwa kushirikiana na sekta binafsi.

Hayo yalisemwa Alhamisi, Oktoba 16, 2025 wakati wa kikao kazi kati ya Ofisi ya Msajili wa Hazina, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Ofisi ya Wakili Mkuu wa Serikali na Ofisi ya Mwandishi Mkuu wa Sheria, kilichofanyika Kibaha, mkoani Pwani.

Msajili wa Hazina Bw. Nehemiah Mchechu alisema maagizo waliyopewa na Mhe. Rais. Dk. Samia Suluhu Hassan, ni uboreshwaji wa sheria ili ziendane na maono yaliyomo kwenye Dira 2050.

“Tunapaswa kuwa na sheria ambazo zitaongeza ufanisi wa taasisi za umma. Tunapaswa kuwa na sheria ambazo zitatoa wigo kwa sekta za umma kufanya kazi kwa ukaribu na sekta binafsi,” alisema Bw. Mchechu.

Alisema kuongezeka kwa ufanisi wa sekta za umma, kutapelekea ongezo la mchango wake kwenye mapato ya ndani ya serikali kutoka asilimia nne ya sasa mpaka kufikia kumi miaka minne ijayo, kama ilivyoelekezwa na Mhe. Rais Samia.

“Tunapaswa kuboresha huduma na bidhaa zetu, pamoja na kupunguza matumizi yasiuyokuwa ya lazima, ili kuongeza mapato na hatimaye gawio kwa serikali,” alisisitiza Bw. Mchechu.

Serikali inataka kuona tija katika uwekezaji wake wa Sh92.3 trilioni ilioufanya katika taasisi za umma na kampuni ambazo ina umiliki wa hisa chache.

Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mhe. Samwel Maneno alisema kuwa uimara wa taasisi za umma na sekta binafasi unategemea ubora wa sheria zinazosimamia uwekezaji.

Alieleza kuwa usimamizi wa mikataba ya uwekezaji usipokuwa mzuri, itakuwa ngumu au itachukua muda mrefu kufikia matarajio yaliyowekwa na serikali.

“Aidha, hali hii inaweza kuibua migogoro na hivyo kupelekea kuwakatisha tamaa wawekezaji,” alisema huku akibainisha kuwa serikali haiko tayari kufikia hatua hiyo.

“Eneo hili la usimamizi wa mikataba tunalipa kipaumbele kikubwa. Kwa mwaka mmoja wa fedha tunaweza kusimamia kati ya mitaba 15,000 na 20,000.

“Na ili kufanya usimamizi wa mikataba hii uwe wa ufanisi, tumeona haja ya kukumbatia matumizi ya teknolojia ili kurahisisha ufuatiliaji.”

Aidha, alielezea haja ya kuepuka urasimu usiokuwa wa lazima ili wawekezaji, hasa katika eneo la ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta Binafsi (PPP).

Kwa upande wake Wakili Mkuu wa Serikali Dk. Ally Possi, alisema sheria za nchi hazitakiwa ziwe kikwazo kwa wawekezaji, badala yake kivutio.

“Ili ndoto yetu ya kuwa na uchumi unaofikia $1 trilioni, ifikie, tunapaswa kuendelea kutengeneza mazingira rafiki ya biashara yatakayovutia wawekezaji zaidi,” alisema.

Sanjari na hilo, Dk. Possi alisema nchi inapaswa kuendelea kuboresha usimamizi wa mikataba, hususani katika eneo la PPP.

Aidha, alisema taasisi za umma zina jukumu la kutoa gawio na kukuza Uchumi wa nchi.

“Lakini hili haliwezi kutimia ikiwa taasisi hizo zitagubikwa na kesi ambazo zitazilazimu kulipa fedha baada ya hukumu ya mahakama kutolewa, na ni katika muktadha huo tumekutana kujadili namna bora ya kukabiliana na mapungufu ya kisheria,” alihitimisha Dk. Possi.

Naye Mwandishi Mkuu wa Sheria Bw. Onorius Njole alisema kufikia Uchumi wa $1 trilioni unategemea uimara wa taasisi za umma na ndio maana ipo haja ya kuwa na mfumo imara wa kisheria katika eneo la uwekezaji.

“Ni lazima mashirika ya umma yasimamiwe na sheria za uwekezaji ambazo zinaendana na mahitaji ya sasa,” alisema.
“Mfumo wa sheria lazima uendane na kasi ya ukuaji wa uwekezaji katika mashirika ya umma.”

SERIKALI YAAHIDI SHERIA RAFIKI KWA WAWEKEZAJI KUFANIKISHA DIRA 2050

Поделиться в:

Доступные форматы для скачивания:

Скачать видео mp4

  • Информация по загрузке:

Скачать аудио mp3

Похожие видео

Northern Corridor - Connecting Rwanda to Global Opportunities

Northern Corridor - Connecting Rwanda to Global Opportunities

🔴#Live: CHALAMILA ANAFICHUA UKWELI VIDEO ZINAZOSAMBAZWA za WANAJESHI na WANANCHI WAKIANDAMANA...

🔴#Live: CHALAMILA ANAFICHUA UKWELI VIDEO ZINAZOSAMBAZWA za WANAJESHI na WANANCHI WAKIANDAMANA...

HALI ILIVYO MUDA HUU MAENEO MBALIMBALI YA MBAGALA MAPEMA LEO DEC 09

HALI ILIVYO MUDA HUU MAENEO MBALIMBALI YA MBAGALA MAPEMA LEO DEC 09

💥 Европа ГОТОВИТ финансовый УДАР по России: активы Кремля пойдут в заем Украине

💥 Европа ГОТОВИТ финансовый УДАР по России: активы Кремля пойдут в заем Украине

Waziri wa Viwanda na Biashara atembelea ofisi ya TBS

Waziri wa Viwanda na Biashara atembelea ofisi ya TBS

#MariaSpaces - #D9 updates and way forward

#MariaSpaces - #D9 updates and way forward

SUGU na PETER MSIGWA WAMFUNGULIA KESI MWANASHERIA MKUU wa SERIKALI...

SUGU na PETER MSIGWA WAMFUNGULIA KESI MWANASHERIA MKUU wa SERIKALI...

Zatajone tożsamości. Fałszywe nazwiska, które zmieniły Polskę

Zatajone tożsamości. Fałszywe nazwiska, które zmieniły Polskę

TOÀN CẢNH 17H 9/12: Gia đình 13 người gặp nạn sau đám cưới | Thông tin tang lễ diễn viên Thương Tín

TOÀN CẢNH 17H 9/12: Gia đình 13 người gặp nạn sau đám cưới | Thông tin tang lễ diễn viên Thương Tín

⚡️

⚡️ "Репарационный КРЕДИТ" и АКТИВЫ РФ: ЕС не может ОТТЯГИВАТЬ решения

18 МЕГАПРОЕКТОВ КИТАЯ, КОТОРЫЕ ИЗМЕНЯТ МИР

18 МЕГАПРОЕКТОВ КИТАЯ, КОТОРЫЕ ИЗМЕНЯТ МИР

Жириновский о евреях! Что будет, когда Израиль проиграет? 2004 год

Жириновский о евреях! Что будет, когда Израиль проиграет? 2004 год

WETOMAT, NOMINACJE AMBASADORÓW I SPOWIEDŹ STANOWSKIEGO. NAJLEPSZE FRAGMENTY WYWIADU Z NAWROCKIM

WETOMAT, NOMINACJE AMBASADORÓW I SPOWIEDŹ STANOWSKIEGO. NAJLEPSZE FRAGMENTY WYWIADU Z NAWROCKIM

SKANDALICZNY WYKŁAD W WARSZAWIE. JAK ZAREAGUJĄ POLSKIE WŁADZE?

SKANDALICZNY WYKŁAD W WARSZAWIE. JAK ZAREAGUJĄ POLSKIE WŁADZE?

Список запретов в России на 2026 год – Как это коснется каждого?

Список запретов в России на 2026 год – Как это коснется каждого?

💥 Годовщина СВЕРЖЕНИЯ РЕЖИМА Асада в Сирии: что изменилось в стране?

💥 Годовщина СВЕРЖЕНИЯ РЕЖИМА Асада в Сирии: что изменилось в стране?

Mwanzo Mwisho Hotuba ya Rais wa TLS Wakili Boniface Mwabukusi kwa Mawakili Wapya

Mwanzo Mwisho Hotuba ya Rais wa TLS Wakili Boniface Mwabukusi kwa Mawakili Wapya

[🔴 Live] Công an Nghệ An tiếp nhận đơn tố cáo liên quan dự án “nuôi em” | Tin tức Mekong 09.12.2025

[🔴 Live] Công an Nghệ An tiếp nhận đơn tố cáo liên quan dự án “nuôi em” | Tin tức Mekong 09.12.2025

Китай показал первый летающий автомобиль в мире, только взгляните…

Китай показал первый летающий автомобиль в мире, только взгляните…

Шум в ушах исчезнет: забытый советский метод, который работает лучше таблеток

Шум в ушах исчезнет: забытый советский метод, который работает лучше таблеток

© 2025 dtub. Все права защищены.



  • Контакты
  • О нас
  • Политика конфиденциальности



Контакты для правообладателей: [email protected]