MUHIMBILI YAOKOA TZS 3.96 BILIONI NDANI YA MIEZI 10
Автор: Kajunason TV
Загружено: 2018-09-09
Просмотров: 46
Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG.
*Wagonjwa 45 wahudumiwa, wagharimu Tshs. 360 Mil. badala ya Tshs. 4.320 Bil kama wangeenda nje ya nchi
*Mmoja agharimu Tshs. 8 Mil. badala ya Tshs. 96 Mil. nje ya nchi
Hospitali ya Taifa Muhimbili imeanzisha kwa mara ya kwanza hapa nchini utoaji wa huduma za tiba radiolojia (Interventional Radiology) ambapo kabla ya uanzishwaji wake wagonjwa waliokuwa wanahitaji huduma hizi walikuwa wakienda nje ya nchi.
Akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam wakati akielezea kuanzishwa wa huduma hiyo, Mkurugenzi wa wa huduma za Tiba Shirikishi Dkt. Praxeda Agweyo amesema kuwa tiba hiyo inahusisha utalaam wa kutumia vifaa vya radiolojia kama X-Ray, MRI, CT-Scan na Ultra-Sound kutibu moja kwa moja ugonjwa au kuchukua sampuli kwa ajili ya uchunguzi.
Amesema kuwa huduma ambazo zimeanza kutolewa kupitia njia hiyo kwa sasa ni kuondoa uvimbe kwenye sehemu ya kinywa, uso na shingoni (sclerotherapy for haemangioma and lymphangioma), kuweka mirija kwenye figo ambazo mirija ya kutoa mkojo imeziba (nephrostomy tube placement), kuzibua mirija ya nyongo iliyoziba (percutaneous trans hepatic biliary drainage) na kuzibua mirija ya uzazi iliyoziba (fallopian tube recanalization). Tiba nyingine ni kunyonya usaha ndani ya tumbo (abscesses drainage).
Ameongeza kuwa wastani wa mgonjwa mmoja kutibiwa uvimbe kwenye sehemu ya kinywa (sclerotherapy for haemangioma) inagharimu kiasi cha Tshs. 2 mil. ambapo kutokana na ugonjwa huo mgonjwa anahitaji kutibiwa hatua nne ili kukamilisha mzunguko wa tiba hiyo sawa na Tshs. 8 mil.
"Mgonjwa kama huyo alipokuwa akienda nje ya nchi ilikuwa inagharimu kiasi cha Tshs. 24 mil. kwa kila hatua moja sawa na Tshs. 96 mil. kwa hatua zote nne," amesema Dkt. Ongweyo.
Tangu kuanzishwa kwa huduma hizi Novemba 2017, jumla ya wagonjwa 45 wamenufaika kwa gharama ya Tshs. 360 mil. sawa na Tshs. 8 mil. kwa kila mgonjwa. Kama wangeenda nje ya nchi ingeigharimu Serikali kiasi cha Tshs. 4.320 Bil. sawa na Tshs. 96 mil. kwa kila mgonjwa.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: