TRA YABAINI 'TRICK' WENYE MALORI YA MAFUTA WAFANYABIASHARA WAWILI WAPANDISHWA KIZIMBANI MKOA SONGWE
Автор: MbeyaYetuOnlineTV
Загружено: 2025-09-11
Просмотров: 5755
#mbeyayetutv
Wafanyabiashara Joseph Petro Mwangere (45) mkazi wa Majengo mjini Tunduma mkoani Songwe Mkurugenzi wa kampuni ya HIKE INVESTMENT LIMITED na Juhudi Boniface Kastom (35) mkazi wa Kinyerezi Jijini Dar es Salaam Mkurungenzi kampuni ya Blue Oceanic Logistic wamepandishwa kizimbani kwa mashtaka ya kukwepa kodi na kusababishia hasara Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA jumla ya Shilingi Mil 75,518,744.
Akisoma Mashtaka mbele ya hakimu Mkazi Mkuu Mfawidhi mkoa wa Songwe Francis Kishenyi, Wakili wa serikali Auni Chilamula aliyeambatana na Wakili mwenzie wa serikali Medalakini Emmanuel ameainisha jumla ya Mashtaka 9, ambapo shtaka la kwanza na la pili ni kukwepa Kodi kwa njia ya Udanganyifu kinyume cha kifungu nambari 203 cha sheria ya Forodha ya Jumuiya Afrika mashariki ya mwaka 2004 maelezo ya kosa yakiwa ni washitakiwa walichepusha mzigo maeneo ya Isongole wilayani Ileje na Majengo mjini Tunduma wilayani Momba.
Wakili Chilamula amesema Shtaka la tatu na la Nne linalowakabili washitakiwa hao Wafanyabiashara Joseph Mwangele na Juhudi Boniface kwamba mnamo tar 23 /08/2025 washitakiwa hao kwa pamoja walichepusha mzigo wa mafuta aina ya Petrol jumla ya Lita elfu 37 uliokuwa ukielekea Nchini Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo na kuushusha maeneo ya Isongole wilayani Ileje na Majengo mjini Tunduma wilayani Momba mkoani Songwe.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: