RAIS SAMIA AIPA TANROADS ZAIDI YA BILIONI 500 UJENZI MIUNDOMBINU DAR ES SALAAM
Автор: Wizara ya Ujenzi
Загружено: 2024-11-10
Просмотров: 3766
Katika kipindi cha miaka mitatu ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan zaidi ya Shilingi Bilioni 500 zimetolewa kwa Wakala ya Barabara Tanzania-TANROADS Mkoani Dar es salaam.
Licha ya kusimamia matengenezo ya barabara na madaraja, katika kipindi cha miaka mitatu Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia imeendelea kutoa fedha kwa ajili ya miradi ya Kimkakati ambayo utekelezaji wake upo kwenye hatua mbalimbali sambamba na kuhakikisha mtandao wa kilomita 619 za barabara zinazosimamiwa na TANROADS zinapitika wakati wote.
Hayo yameelezwa na Meneja wa Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) Mkoa wa Dar es salaam Mhandisi John Mkumbo leo tarehe 8 Novemba 2024 wakati akitoa ufafanuzi kuhusu utekelezaji wa miradi ya barabara, madaraja pamoja na vivuko katika mkoa huo.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: