Ni Aibu! Msitu wa Ngezi Unaleta Milioni 15 Tu kwa Mwaka? Tunahitaji Kuamka!
Автор: kilimo tv
Загружено: 2025-12-07
Просмотров: 1121
Waziri wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo, Mhe. Suleiman Masoud Makame, ameonesha kutoridhishwa na kiwango kidogo cha mapato yanayotokana na wageni wanaotembelea Hifadhi ya Ngezi.
Amesema ukusanyaji wa takribani shilingi milioni 15 kwa mwaka ni mdogo sana na haufanani na fursa kubwa ya utalii iliyopo katika hifadhi hiyo.
Waziri Makame amewataka watendaji kusimamia kikamilifu rasilimali zilizopo na kubuni mbinu mpya na za kisasa za kuvutia watalii zaidi, ili kuongeza mapato na kuchangia katika ustawi wa uchumi wa Taifa.
Kwa sasa, mapato yanayotokana na ugeni katika Hifadhi ya Ngezi yamebaki katika kiwango cha shilingi milioni 15 kwa mwaka, hali ambayo amesema haiakisi thamani kubwa ya hifadhi hiyo.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: