NILITAMANI: Mapambazuko ya Machweo na Hadithi Nyingine.
Автор: Simon Maina HSC
Загружено: 2025-08-24
Просмотров: 2722
Nilitamani ni hadithi inayomhusu msichana mmoja kwa jina Tumaini. Tumaini anatoka nchini kwao, Kenya, na kwenda katika nchi jirani, Tanzania, ili akatafute riziki kutokana na umaskini uliomkumba. Anamwacha mwanawe na bibi yake, Farida.
Anapoenda Tanzania, anapata marafiki wanaomfaa sana, ikiwemo Nina na Jenifa. Tumaini anatamani sana maisha ya Nina kwa kuwa Nina alikuwa na mume mzuri kwa hali na mali. Wakati mmoja alipokuwa anabarizi katika Coco Beach, anapatana na kijana mtanashati kwa jina Romeo, aliyedhani angemwoa na kuishi maisha ya kitajiri. Hata hivyo, inatokea kuwa Romeo hakuwa binadamu wa kawaida ila alikuwa jini.
Baadhi ya maudhui yanayojitokeza ni pamoja na:
1. Tamaa
2. Umaskini
3. Utabaka
4. Utu
5. Ukatili
6. Matumaini
n.k.
Maswali:
a) Eleza umuhimu wa mhusika Tumaini katika kuendeleza hadithi ya Nilitamani. (Alama 10)
b) "Tamaa mbele mauti nyuma". Jadili ukweli wa kauli hii kwa kurejelea hadithi hii. (Alama 10)
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: