RAIS MAGUFULI AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA HOSPITALI TUNDUMA& BARABARA YA MPEMBA-ISONGOLE KM50.3
Автор: Ikulu Tanzania
Загружено: 2019-10-04
Просмотров: 14616
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 05 Oktoba, 2019 ameweka mawe ya msingi katika miradi miwili ya ujenzi wa Hospitali ya Mji wa Tunduma na ujenzi wa barabara ya lami ya Mpemba – Isongole inayounganisha Tanzania na Malawi.
Jengo la Hospitali ya Mji wa Tunduma yenye hadhi ya Hospitali ya Wilaya linajengwa kwa gharama ya shilingi Bilioni 4.9 ambapo mpaka sasa ujenzi wake umegharimu shilingi Bilioni 2.2.
Barabara ya Mpemba – Isongole ina urefu wa kilometa 50.3, inajengwa kwa kiwango cha lami kuunganisha Tanzania na Malawi kwa gharama ya shilingi Bilioni 109.439 na ujenzi wake umefikia asilimia 48.
Akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika Mjini Tunduma, Mhe. Rais Magufuli amempongeza Meneja wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) katika Mkoa wa Songwe kwa ujenzi bora wa jengo la Hospitali ya Mji wa Tunduma na ameagiza fedha zilizobaki kwa ajili ya kukamilisha mradi huo zitolewe haraka ili hospitali ikamilike na kuanza kutoa huduma kwa wananchi.
Mhe. Rais Magufuli amesema kujengwa kwa hospitali hiyo pamoja na hospitali ya Uhuru Mkoani Dodoma kunafanya idadi ya hospitali mpya zinazojengwa tangu Serikali ya Awamu ya Tano iingie madarakani kufikia 69 na kwamba lengo la kujengwa kwa hospitali hizo pamoja na vituo vya afya vipya 352 kunalenga kuwaondolea Watanzania adha ya kupata matibabu.
Kuhusu ujenzi wa barabara ya Mpemba – Isongole, Mhe. Rais Magufuli ameelezea kutoridhishwa na kasi ndogo ya mkandarasi China GEO Engineering anayejenga barabara hiyo ambaye ameanza kazi mwaka 2017 na ameagiza kuanzia sasa kazi za ujenzi zifanyike usiku na mchana ili mradi ukamilike kwa wakati, vinginevyo hatua zichukuliwe dhidi ya mkandarasi huyo.
Mhe. Rais Magufuli pia ameelezea kutofurahishwa na gharama kubwa za ujenzi wa barabara hiyo ambapo wastani wa kilometa 1 ni takribani shilingi Bilioni 2 na hivyo ametaka kuanzia sasa asiwe anaalikwa kuweka mawe ya msingi ama kufungua miradi ambayo gharama zake za ujenzi ni kubwa kupita kiasi.
Wakizungumza katika mkutano huo Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Selemani Jafo na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mhe. Ummy Mwalimu wamemshukuru Mhe. Rais Magufuli kwa uwekezaji mkubwa anaoufanya katika sekta ya afya hali iliyosaidia kusogeza huduma za matibabu jirani na wananchi, kupunguza vifo vya akina mama wajawazito wakati wa kujifungua na kuimarisha upatikanaji wa dawa.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mhe. Isack Kamwelwe amesema pamoja na kujengwa kwa kiwango cha lami kwa barabara ya Mpemba – Isongole, Serikali imejenga barabara nyingine zaidi ya 10 katika ukanda wa Nyanda za Juu Kusini zikiwemo Sumbawanga – Kanazi (km 75), Kanazi – Kizi – Kibaoni (km 76.7), Sitalike – Mpanda (km 36.7), Sumbawanga – Matai – Kasanga (km 112), Mbeya – Lwanjilo (km 36), Kikusa – Ipinda – Matema (km 39.1), Lwanjilo – Chunya (km 36), Chunya – Makongorosi (km 39), Njombe – Moronga (km 53.9), Njombe – Makete (km 53.5), Lusitu – Mawengi (km 50) na daraja la Momba (lenye urefu wa meta 84).
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: