SUMAYE AKIFAFANUA UUZWAJI WA NYUMBA SERIKALI SWALI LA SAED KUBENEA
Автор: Grann Chaco
Загружено: 2015-06-03
Просмотров: 29263
Frederick Sumaye alipotangaza nia ya kugombea na kujibu maswali ya waandishi. Swali hili pia amekuwa akiulizwa sana na waziri Dkt. Magufuli
Swali : Ukiwa Waziri Mkuu serikalini ndio nyumba za serikali ziliuzwa kwa bei ya kutupwa, unasemaje kuhusu hili?
Jibu: uuzwaji wa nyumba za serikali, Rais alishauri na Baraza la Mawaziri akakubali. Kuna tume tatu zilifanyia kazi suala hili kwa muda tofauti na zote zilikuja na mapendekezo kuwa nyumba za serikali ni nyingi na serikali inagharamia fedha nyingi kuzikarabati na hivyo tuwauzie watumishi wa Umma.
Tulikuwa na nyumba nyingi mfano Breweries na bandari walikuwa na nyumba zaidi ya elfu moja. Nyumba nyingi zilinunuliwa mpaka na wananchi wa kawaida, Rais alishituka kuona ghorofa zinainuka Oysterbay zilipokuwepo nyumba za serikali.
Rais akasema lazima waraka uandikwe wauziwe wafanyakazi waliokuwa wakiishi humo na hakuna kuuzwa mpaka baada ya miaka 25 kulingana na mkataba wa manunuzi, na serikali ndio ilifanya tathmini na watumishi wa serikali wadogo kabisa wakauziwa.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: