MULIRO AKABIDHI ASKARI WA KIKE BENDERA KWA NIABA YA IGP KWENDA SCOTLAND.
Автор: BETE TV
Загружено: 2025-09-04
Просмотров: 134
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Jumanne Muliro amewakabidhi bendera ya Taifa askari wa kike kwa niaba ya Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini IGP Camillus Wambura wanaokwenda katika mafunzo ya shirikisho la askari wa kike duniani (IAWP) nchini Scotland.
Amesema kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini anathamini mchango wa shirikisho hilo ambalo limesaidia sana kuleta chachu ya mabadiliko ya kiutendaji ndani ya Jeshi la Polisi tangu waanze kushiriki mafunzo hayo katika maeneo tofauti tofauti duniani.
Aidha Kamanda Muliro amesisitiza kuwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini amewataka maafisa na askari hao wanaokwenda nchini Scotland kuwa na nidhamu muda wote wa mafunzo kama ilivyo kauli mbiu ya Jeshi la Polisi Tanzania, nidhamu haki weledi na uadilifu.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: