Mwanzo Mwisho wa tukio la SABAYA kwenda kutoa shukrani KANISANI
Автор: Mwananchi Digital
Загружено: 2024-02-04
Просмотров: 3344
Arusha. Baadhi ya wananchi wamempongeza aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai,Lengai Ole Sabaya kwa kuonyesha unyenyekevu na kumtakia heri katika maisha yake mapya, huku wengine wakimsifu kwa kauli aliyoitoa ya kuwasamehe wote waliomkosea.
Aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai, Lengai ole Sabaya leo Jumapili February 4,2024 amewaomba msamaha wote aliowakosea na kusema amewasamehe wale wote waliomkosea huku akiwaomba msamaha aliyowakosea pia.
Sabaya alitoa msamaha huo katika ibada ya shukrani iliyofanyika katika kanisa la Ebenezer Restoration Ministry of all Nation Moshono Jijini Arusha, baada ya kuachiwa huru na mahakama kwa makosa mbalimbali yaliyokuwa yakimkabili.
Msamaha wa Sabaya umepokelewa kwa hisia tofauti na wananchi mbalimbali, ambao wametoa maoni yao kupitia Mwananchi Digital kwamba ni kauli ya kiungwana na unyenyekevu yenye funzo kubwa maishani kwamba hupaswi kukata tamaa kipindi unapitia hatua ngumu.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: