MABAKI YA MWILI WA NAOMI ALIYEULIWA NA MUMEWE, YAZIKWA KILIMANJARO BAADA YA KUKAA ZAIDI YA MIAKA 5
Автор: Mwananchi Digital
Загружено: 2025-03-15
Просмотров: 6594
Mwanga. Wakati mabaki ya mwili wa Naomi Marijani (36) aliyeuawa na mumewe yakizikwa baada ya kukaa kwa zaidi ya miaka mitano, ndugu wa familia yake wamesema wanamshukuru Mungu.
Naomi ambaye ameacha mtoto mmoja wa kike, aliuawa Machi 15, mwaka 2019 jijini Dar es salaam na mumewe, Hamis Luwongo na kisha akauchoma moto mwili wake kwa kutumia magunia mawili ya mkaa ndani ya banda la kuku.
Kisha masalia ya mwili na majivu alikwenda kuyazika shambani na kupanda migomba juu yake.
Hata hivyo, Februari 26, mwaka huu, Mahakama kuu Kanda ya Dar es salaam ilimuhukumu kunyongwa hadi kufa baada ya kukutwa na hatia ya kumuua mke wake huyo.
Akizungumza wakati wa kuaga mwili wa Naomi, baba mdogo wa marehemu, Robert Marijani amewashukuru wote waliohusika kupambania haki ya mtoto wao Naomi na kusema mengine wanamshukuru Mungu.
Akisoma historia fupi ya marehemu, kaka wa marehemu, Ismail Marijani, amesema dada yao alikuwa ni mtu mwema kwao na kwa wengine na kwamba alikuwa ni mpenda haki, hivyo watamkumbuka kwa mengi.
Akimzungumzia Naomi, Mchungaji wa Kanisa la Gezaulole-TAG, Mchungaji Jacob Chinegu amesema Naomi alikuwa ni mwanamke mpambanaji na alishiriki katika matukio ya kanisa.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: