WAZIRI MKENDA Atembelea Kiwanda Cha Kuchakata Mafuta ya Mawese Kisiwani Kalangala-Uganda
Автор: WazoHuru Media
Загружено: 2021-11-25
Просмотров: 1669
Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Kilimo imejipanga katika kuhakikisha inampatia mwekezaji eneo la kuwekeza kwenye zao la michikichi, kutoa elimu kwa wakulima na kuwasaidia kifedha ili kuhakikisha nchi inapunguza ama kumaliza kabisa kadhia ya kuagiza mafuta ya mawese kutoka nje ya nchi.
Hayo yamebainishwa na Waziri wa Kilimo Mhe. Prof Adolf Mkenda tarehe 25 Novemba 2021 wakati alipotembelea kiwanda cha kuchakata mafuta cha kampuni ya Oil Palm Uganda Limited kilichopo katika kisiwa cha Kalangala nchini Uganda wakati akiwa katika ziara ya kikazi ya siku nne nchini humo.
Waziri Mkenda amesema kuwa Serikali ya Tanzania itaimarisha mfumo wa kilimo cha Michikichi kwa kuhakikisha kuwa inatoa elimu ya kutosha kwa wakulima kwa utaratibu ambao utahusisha mashamba makubwa na mashamba ya wakulima wadogo ili kuwa na kilimo chenye tija kinachowakikishia soko kwenye viwanda.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: