Ubora wa sunna ya kuchinja na hukmu zake
Автор: Kituo Cha Kiislamu Cha Kimisri
Загружено: 2020-07-26
Просмотров: 5854
Basi swali kwa ajili ya Rabb wako na chinja kwa ajili Yake.
[Al-Kawthar: 2]
لَن يَنَالَ اللَّـهَ لُحُومُهَا وَلَا دِمَاؤُهَا وَلَـٰكِن يَنَالُهُ التَّقْوَىٰ مِنكُمْ ۚ كَذَٰلِكَ سَخَّرَهَا لَكُمْ لِتُكَبِّرُوا اللَّـهَ عَلَىٰ مَا هَدَاكُمْ ۗ وَبَشِّرِ الْمُحْسِنِينَ ﴿٣٧﴾
37. Haimfikii Allaah nyama zake wala damu yake, lakini inamfikia taqwa kutoka kwenu. Hivyo ndivyo Tulivyowatiisha kwenu ili mpate kumtukuza Allaah; Allaahu Akbar, kwa yale Aliyokuongozeni; na wabashirie wafanyao ihsaan. [Al-Hajj: 37]
Kutoka kwa mama wa Waumini 'Aaishah (Radhwiya Allaahu anhaa) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakuna kitendo cha mwana Aadam kilichokuwa ni kipenzi kabisa kwa Allaah siku ya kuchinja kama kumwaga damu (kuchinja). Atakuja (huyo mnyama) siku ya Qiyaamah na pembe zake, kucha zake na nywele zake. Damu yake itamwagika mahali fulani Allaah Anapajua kabla ya kumwagika katika ardhi. Hivyo zipendezesheni nafsi kwayo)) [At-Tirmidhiy]
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: