Ziara ya Uongozi wa ZPC katika Mradi wa CBM Bandari ya Mangapwani
Автор: Shirika la Bandari Zanzibar
Загружено: 2025-08-27
Просмотров: 1988
Ziara ya Uongozi wa ZPC katika Mradi wa CBM Bandari ya Mangapwani
Uongozi wa Shirika la Bandari Zanzibar (ZPC) umefanya ziara ya ukaguzi katika Mradi wa Conventional Buoy Mooring (CBM) wa upakiaji na ushushaji wa mafuta na gesi unaoendelea katika Bandari ya Mangapwani.
Katika ziara hiyo, wamekagua na kushuhudia hatua za maandalizi ya ufungaji wa vifaa muhimu vikiwemo:
Maboya (Buoys) 6, kila moja yakiwa na uwezo wa kuhimili uzito wa zaidi ya tani 150.
Sinkers zenye uzito wa zaidi ya tani 5 kila moja kwa ajili ya kuimarisha uthabiti wa maboya hayo.
Mfumo wa kisasa wa Coriolis Flow Meter kwa ajili ya kufuatilia mtiririko na kupima kiwango cha mafuta ya yatakayopitishwa.
Mfumo wa Scudder System, unaohusiana na usalama na uthabiti wa meli wakati wa upakiaji na ushushaji.
Jengo la Ofisi za Wadau wa Sekta ya Mafuta, litakalotumika kama kituo cha uratibu wa shughuli zote za mradi.
Mradi huu wa kimkakati unatarajiwa kuongeza ufanisi na usalama wa miamala ya mafuta Zanzibar, sambamba na kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia sekta ya bandari na nishati.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: