HII NDIO BARABARA YA MCHEPUO 'MLIMA WA NYOKA' // TAZAMA IKIPANULIWA, NI KWENYE BARABARA YA TANZAM
Загружено: 2026-01-20
Просмотров: 1289
Serikali kupitia Wakala ya Barabara Tanzania (TANROADS) imeanza upanuzi na ujenzi wa barabara ya mchepuo katika eneo la Mlima Nyoka lililopo kwenye barabara ya TANZAM, kwa lengo la kupunguza ajali za mara kwa mara, msongamano wa magari na kuongeza usalama kwa watumiaji wa barabara hiyo muhimu kitaifa na kikanda.
Akizungumza kuhusu mradi huo, Meneja wa Barabara Kuu na Barabara za Mijini kutoka TANROADS, Mhandisi Nchama Wambura, amesema kuwa uamuzi wa kupanua barabara hiyo umetokana na ongezeko kubwa la magari, hususan malori makubwa, ambayo yamekuwa yakikumbwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kushindwa kupanda Mlima Nyoka na kusababisha ajali zinazoharibu mali na kupoteza maisha ya watu.
Mhandisi Wambura amesema Mlima Nyoka ni mrefu na mkali, hali inayosababisha magari mengi kukwama na kusababisha msongamano mkubwa wa magari, jambo lililoilazimu TANROADS kuanzisha ujenzi wa njia ya mchepuo pamoja na maeneo ya magari kupumzikia, ili kurahisisha mtiririko wa magari na kupunguza adha kwa madereva.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: