WAZIRI NDEJEMBI: UTENDAJI WA OSHA UNARIDHISHA
Автор: OSHA TV ONLINE
Загружено: 2024-07-08
Просмотров: 81
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Deogratius Ndejembi, ameeleza kuridhishwa na utendaji wa Mamlaka ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) ambao umeimarika kutokana na matumizi ya mifumo ya TEHAMA ambayo imeboresha na kurahisisha upatikanaji wa huduma za usalama na afya nchini.
Ametoa kauli hiyo, alipotembelea banda la OSHA katika Maonesho ya 48 ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Saba Saba) yanayoendelea katika Viwanja vya Saba Saba vilivyopo Barabara ya Kilwa, Temeke Jijini Dar es Salaam.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: