MABASI YA MWENDOKASI YAMVURUGA WAZIRI MKUU, ATINGA GEREZANI KUKAGUA MWENYEWE, WANAIBA MAPATO SI HAYA
Автор: Millard Ayo
Загружено: 2021-04-19
Просмотров: 96104
Waziri mkuu Kasim majaliwa ametembelea mradi wa usafiri Dar es salaam UDART (Mabasi yaendayo haraka) unaotoa huduma kati ya Gerezani kariakoo na mbezi wilaya ya ubungo na kukuta madudu mengi yakiwepo ya ukusanyaji wa nauli ambao haufanywi kwa ya kielekroniki na magari yao mengi kua mabovu huku vipuri vyake vikiwa havipo kwenye magari hayo.
Hayo ameyabaini baada ya kutembelea kituo cha mabasi yaendayo haraka (mwendokasi) cha Gerezani kariakoo na kukuta ukataji wa tiketi ukiwa unafanyika kwa njia ya kawaida tofauti na ulipaji kwa njia ya kieletroniki ambayo mapato yote yanakua katika mtandao na yanaweza kuwekwa katika kumbukumbu huku kwa miaka isiyopungua mitano kampuni ya UDART hawajawai nunua gari mpya wala kurekebisha mfumo wa ukatishaji kwa njia ya eletronik uanze kufanya kazi.
Akiwa katika karakana ya kurasini ya mabasi ya Mwendokasi UDART waziri mkuu Majaliwa amekuta magari ambayo ni mabovu yametolewa engine zake na vitu vingine huku mkurugenzi mtendaji wa UDART Leonard Lwakatare akimwambia waziri mkuu shida ni upande wa gia box.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: