Популярное

Музыка Кино и Анимация Автомобили Животные Спорт Путешествия Игры Юмор

Интересные видео

2025 Сериалы Трейлеры Новости Как сделать Видеоуроки Diy своими руками

Топ запросов

смотреть а4 schoolboy runaway турецкий сериал смотреть мультфильмы эдисон
dTub
Скачать

THRDC: Tunapochelewa kufanya maridhiano ndivyo mambo yanavyozidi kuwa mengi

Автор: WATETEZI TV

Загружено: 2025-12-05

Просмотров: 70

Описание:

Katika kuelekea mwisho wa mwaka, Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), unaounganisha mashirika takribani 300 nchini, umeshauri mamlaka kuanza mazungumzo ya maridhiano mapema iwezekanavyo badala ya kusubiri Tume maalum iliyoundwa kukamilisha uchunguzi.

Leo, Desemba 5, 2025, Mratibu wa THRDC Kitaifa, Wakili Onesmo Olengurumwa, amesema kuwa kutokana na hali ya sintofahamu iliyopo nchini, mazungumzo ya maridhiano yanapaswa kuanza haraka ili kupunguza mkanganyiko unaoendelea. Amesema kuchelewesha mchakato huo kunazidisha changamoto.

"Tunapochelewa kuingia kwenye maridhiano, kila siku matukio yanaongezeka na kufanya suala la maridhiano kuwa gumu zaidi. Tusipokuwa makini, mambo mengine yataendelea kutokea. Tunapochelewa kuingia kwenye maridhiano, mambo yanakuwa mengi zaidi," amesema Olengurumwa.

Aidha, ameshauri kuwa mchakato wa maridhiano uwe wazi na jumuishi kwa wadau wa makundi yote ya kijamii. Amesisitiza umuhimu wa watu kupewa uhuru wa kusema ukweli ili kuponya Taifa. Ametoa mfano wa Waziri wa Vijana, Joel Nnauka, ambaye kwenye ziara zake huwapa vijana nafasi ya kuzungumza kwa uwazi na ukweli.

Olengurumwa amesema si lazima mchakato huo uongozwe na viongozi wa ndani pekee; badala yake, inawezekana wakapatikana waratibu kutoka mataifa rafiki ambao wanaweza kusaidia kusimamia mchakato huo kwa lengo la kuimarisha umoja wa kitaifa.

Amebainisha kuwa kwa sasa kuna hofu katika makundi mbalimbali kuhusu shughuli zao na maandalizi ya sikukuu za mwisho wa mwaka. Kwa msingi huo, ametaja umuhimu wa kupata suluhu ya haraka ili kuondoa wasiwasi huo.

Aidha amewataka viongozi wote kuzungumza kauli za kuponya na kuunganisha wananchi. Aidha, amewahimiza viongozi wa dini na wadau wengine wanaopata nafasi ya kuzungumza hadharani kuhakikisha wanazingatia hoja madhubuti na kuepuka kueneza misimamo ya kidini ambayo inaweza kuongeza mpasuko.

"Kila anayezungumza na chombo cha habari kwa sasa, ni vyema nia yake iwe kuliponya Taifa. Huu sio muda wa mashindano au kuvutana. Tusivutane kwa kuwa tutaendelea kuliumiza Taifa, tusiendelee kushupaza shingo," amesema Olengurumwa.

Hata hivyo, amesema Mtandao umesikitishwa na ukimya wa wazee waliowahi kuitumikia nchi katika nafasi mbalimbali. Amesema ukimya huo unazua maswali, ikizingatiwa uzoefu na umuhimu wao katika nyakati kama hizi. Amewataka wajitokeze na kutoa ushauri kuhusu hatua zinazoweza kusaidia nchi kutoka ilipo sasa.

Amesema kwamba kufuatia maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan, tayari watuhumiwa 1,146 kati ya 2,045 waliokamatwa wakati na baada ya uchaguzi, na kushtakiwa kwa makosa mbalimbali ikiwemo uhaini, wameachiwa huru baada ya mashtaka yao kufutwa na DPP.

Ametoa wito wa kuwaachia zaidi ya watu 800 wanaodaiwa bado kushikiliwa, pamoja na wale waliokamatwa kutokana na masuala ya kisiasa, akiwemo Tundu Lissu. Amesema kwamba mwendelezo wa jitihada hizo unaleta umoja wa kitaifa.

Aidha, ameongeza kuwa baada ya hatua za kuponya machungu kupigwa, ni muhimu kufumua mifumo ya utawala na uongozi, ikiwemo kukamilisha mchakato wa Katiba Mpya ambayo ndiyo msingi mama wa nchi.

Amesisitiza kuwa kwa sasa sio wakati wa kukamata watu kiholela, kulaumiana au kuvutana. Badala yake, amesema ni muhimu kuendelea kulinda haki za binadamu na kuhakikisha ushirikishwaji mpana wakati Taifa linatafuta muafaka.

Tamko hili linakuja wakati ambao kuemeendelea kuwepo mijadala mbalimbali kwenye mitandao na vyombo vya habari kuhusu mwenendo wa hali ya kisiasa nchini Tanzania kabla na baada ya uchaguzi, ambapo matukio mbalimbali ikiwemo uvunjifu wa haki za binadamu, kauli za viongozi vikiwa sehemu kubwa ya mijadala hiyo.

THRDC: Tunapochelewa kufanya maridhiano ndivyo mambo yanavyozidi kuwa mengi

Поделиться в:

Доступные форматы для скачивания:

Скачать видео mp4

  • Информация по загрузке:

Скачать аудио mp3

Похожие видео

SIRI NZITO ANACHOKIFANYA DP WORLD KWENYE BANDARI YA DAR ES SALAAM, MABILIONI YAOKOLEWA

SIRI NZITO ANACHOKIFANYA DP WORLD KWENYE BANDARI YA DAR ES SALAAM, MABILIONI YAOKOLEWA

ДНК создал Бог? Самые свежие научные данные о строении. Как работает информация для жизни организмов

ДНК создал Бог? Самые свежие научные данные о строении. Как работает информация для жизни организмов

HATUA BORA ZA UANDISHI, KATIKA UFANYAJI WA TAFITI   KAMISHNA DKT. IDD R. MANDI

HATUA BORA ZA UANDISHI, KATIKA UFANYAJI WA TAFITI KAMISHNA DKT. IDD R. MANDI

Mapya Yaibuliwa Kwenye Mgogoro wa Nyumba Mjane Alice na Mohammed Yusufali, Mabaunsa Waitwa Polisi

Mapya Yaibuliwa Kwenye Mgogoro wa Nyumba Mjane Alice na Mohammed Yusufali, Mabaunsa Waitwa Polisi

Крепостное право за 22 минуты

Крепостное право за 22 минуты

MWABUKUSI :

MWABUKUSI : "MAWAKILI ACHENI UOGA, FATA KATIBA INAVYOSEMA" AGUSIA YALIYOTOKEA OKTOBA 29

История Византии за 13 минут

История Византии за 13 минут

KAMISHNA  DKT. IDD MANDI AKIELEZEA KUHUSU SHERIA YA KUANZISHWA KWA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA

KAMISHNA DKT. IDD MANDI AKIELEZEA KUHUSU SHERIA YA KUANZISHWA KWA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA

Bishop Askofu Gwajima|Aongea Juu Ya Muafaka Na Mustakabali Watanzania Kuelekea Uchaguzi Mkuu

Bishop Askofu Gwajima|Aongea Juu Ya Muafaka Na Mustakabali Watanzania Kuelekea Uchaguzi Mkuu

Гайд по лососям. Как выбирать, как солить, как выжать из рыбы всё.

Гайд по лососям. Как выбирать, как солить, как выжать из рыбы всё.

HISTORIA YA IKULU YA MAGOGONI-DAR ES SALAA NA CHAMWINO-DODOMA

HISTORIA YA IKULU YA MAGOGONI-DAR ES SALAA NA CHAMWINO-DODOMA

Шокирующий ОПРОС в Москве! Массовая ДЕГРАДАЦИЯ! РОЖАТЬ не хотят! Почему они ЗА ВОЙНУ? | Палата №200

Шокирующий ОПРОС в Москве! Массовая ДЕГРАДАЦИЯ! РОЖАТЬ не хотят! Почему они ЗА ВОЙНУ? | Палата №200

Жириновский о евреях! Что будет, когда Израиль проиграет? 2004 год

Жириновский о евреях! Что будет, когда Израиль проиграет? 2004 год

Гитлер в цвете

Гитлер в цвете

GOOD NEWS! Mtafaruku Mkubwa CCM | SAMIA Atumia Mashehe Kumshambulia NCHIMBI | Wadai Anatumiwa na TEC

GOOD NEWS! Mtafaruku Mkubwa CCM | SAMIA Atumia Mashehe Kumshambulia NCHIMBI | Wadai Anatumiwa na TEC

Как описана ВТОРАЯ МИРОВАЯ в учебниках ЯПОНИИ

Как описана ВТОРАЯ МИРОВАЯ в учебниках ЯПОНИИ

СЕНСАЦИЯ! Мессинг Видел Будущее 2026 - Власти в Панике

СЕНСАЦИЯ! Мессинг Видел Будущее 2026 - Власти в Панике

🤯В Кремле ПОСЛАЛИ Трампа! Путин СЛИЛ ПЕРЕГОВОРЫ. США СДАЮТ Украину у всех на глазах? ЦИМБАЛЮК

🤯В Кремле ПОСЛАЛИ Трампа! Путин СЛИЛ ПЕРЕГОВОРЫ. США СДАЮТ Украину у всех на глазах? ЦИМБАЛЮК

Геннадий Головкин как с Цепи Сорвался! Такое не Забыть…

Геннадий Головкин как с Цепи Сорвался! Такое не Забыть…

ЧТО СДЕЛАЛ АНДРОПОВ С НАСИЛЬНИКАМИ СВОЕЙ ДОЧЕРИ? КГБ ДЕЙСТВОВАЛ без пощады!

ЧТО СДЕЛАЛ АНДРОПОВ С НАСИЛЬНИКАМИ СВОЕЙ ДОЧЕРИ? КГБ ДЕЙСТВОВАЛ без пощады!

© 2025 dtub. Все права защищены.



  • Контакты
  • О нас
  • Политика конфиденциальности



Контакты для правообладателей: [email protected]