KICHANGA CHATELEKEZWA NYUMBA YA WAGENI NZEGA
Автор: ITV Tanzania
Загружено: 2026-01-19
Просмотров: 735
Mwanamke mmoja asiyejulikana ametelekeza kichanga cha siku tatu katika nyumba ya wageni wilayani Nzega, mkoani Tabora, na kutoweka kusikojulikana.
Tukio hilo limemlazimu Mkuu wa Wilaya ya Nzega, Bi. Naitapwaki Tukai, kutoa wito kwa mzazi huyo ajisalimishe huku akiahidi zawadi ya shilingi laki tano kwa yeyote atakayesaidia kumpata ili mtoto apate haki ya kunyonyeshwa na kulelewa na mama yake.
Mkuu huyo wa wilaya amesisitiza kuwa hana nia ya kumchukulia hatua za kisheria mama huyo, bali amedhamiria kushirikiana naye katika malezi ya mtoto endapo atabainika kuwa na hali duni ya kimaisha.
Amewasihi wananchi kutoa ushirikiano ili kuokoa maisha ya kichanga hicho ambacho kwa sasa kinahitaji upendo na uangalizi wa karibu wa mzazi wake.
Powered by #MCHEZOSUPA
JINSI YA KUSHIRIKI MCHEZO SUPA:
-
Tuma 1000 kupitia Airtel Money, Tigo Pesa, M - Pesa, Halopesa, kwenda namba ya kampuni 222223 kumbukumbu namba ni 777 au weka neno ITV.
#ITVDigital #ITVUpdates #ITVTanzania
#Follow @itvtz @radioonetanzania
@capitaldigitaltanzania.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: