OSHA WAFUNDWA MASUALA YA KIUTENDAJI.
Автор: OSHA TV ONLINE
Загружено: 2024-12-20
Просмотров: 65
Watumishi wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA) wametakiwa kuzingatia weledi katika kutekeleza jukumu lao la msingi la kusimamia usalama na afya mahali pa kazi ili kuwahakikishia wananchi upatikanaji wa huduma bora.
Wito huo umetolewa na Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Bi. Mary Maganga, alipokuwa akifunga Kikao cha Tatu cha Baraza la Tano la Wafanyakazi wa OSHA kilichohitimishwa jana (Desemba 19, 2024) Jijini Arusha.
Akiwasilisha hotuba yake ya kufunga kikao tajwa, Katibu Mkuu, Bi. Mary Maganga, amesema kwakuzingatia wajibu wa OSHA wa kuzuia ajali, magonjwa na vifo mahali pa kazi, utekelezaji wa majukumu husika unahitaji weledi wa hali ya juu.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: