UJENZI BANDARI YA MARUHUBI (MPIGADURI) MBIONI KUKAMILIKA
Автор: ASAM Online TV
Загружено: 2026-01-12
Просмотров: 3932
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, amesema ujenzi wa Bandari ya Maruhubi (Mpigaduri) unalenga kutekeleza dira ya kukuza uchumi wa buluu na kuifanya Zanzibar kuwa kitovu cha biashara na utalii katika ukanda wa Afrika Mashariki na Bahari ya Hindi.
Amesema hayo kwa niaba ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, katika hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa bandari hiyo ya abiria na mizigo, iliyofanyika Mkoa wa Mjini Magharibi.
Ameeleza kuwa Bandari ya Maruhubi imepangwa kuwa Triport ya kwanza Afrika Mashariki, itakayotoa huduma za meli za abiria, teksi na ndege za baharini, pamoja na kituo cha mabasi, hoteli ya nyota tano na jengo la biashara, hatua itakayochochea ukuaji wa uchumi na biashara nchini.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: