Популярное

Музыка Кино и Анимация Автомобили Животные Спорт Путешествия Игры Юмор

Интересные видео

2025 Сериалы Трейлеры Новости Как сделать Видеоуроки Diy своими руками

Топ запросов

смотреть а4 schoolboy runaway турецкий сериал смотреть мультфильмы эдисон
dTub
Скачать

IRINGA KUTOA CHANJO KWA NG’OMBE ZAIDI YA LAKI NNE KATIKA KAMPENI YA TAIFA YA CHANJO YA MIFUGO

Автор: PAMLOMO24

Загружено: 2025-11-07

Просмотров: 35

Описание:

Serikali imeanza utekelezaji wa kampeni ya kitaifa ya chanjo na utambuzi wa mifugo kwa kipindi cha miaka mitano (2025–2029), ambapo Mkoa wa Iringa unatarajia kuchanja ng’ombe zaidi ya 400,000, mbuzi na kondoo 20,000, pamoja na kuku milioni 1.5 katika kampeni hiyo.
Afisa Mfawidhi wa Kituo cha Uchunguzi wa Magonjwa ya Mifugo Kanda ya Nyanda za Juu Kusini (ZVC–Iringa), Dk. Jeremiah Choga, amesema kampeni hiyo, iliyoanza Juni mwaka huu chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, inalenga kudhibiti magonjwa ya mifugo na kuongeza tija katika sekta hiyo.
“Kama inavyofahamika, sekta ya mifugo hukabiliwa na magonjwa mengi. Serikali kupitia wizara imetenga fedha kwa ajili ya kutoa chanjo dhidi ya magonjwa mbalimbali. Kampeni hii ya miaka mitano hadi mwaka 2029 imeanza kwa kuchanja ng’ombe dhidi ya homa ya mapafu, huku maeneo mengine yakihusisha mbuzi, kondoo na kuku,” alisema Dk. Choga.
Aliongeza kuwa serikali imetenga shilingi bilioni 216 kwa ajili ya utekelezaji wa kampeni hiyo, ambayo pia inahusisha kuvalisha mifugo heleni za utambuzi ili kudhibiti wizi na kuboresha usimamizi wa takwimu za sekta hiyo.
“Faida za kampeni hii ni pamoja na kujua idadi halisi ya mifugo nchini, kupunguza magonjwa, kuboresha afya ya mifugo na kuongeza uzalishaji wa mazao ya mifugo,” alifafanua.
Katika Halmashauri ya Mji wa Mafinga, zaidi ya ng’ombe 8,000 sawa na asilimia 88 ya lengo tayari wamepatiwa chanjo, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kupambana na magonjwa ya mifugo.
Dk. Aldonis Ulimboka, Daktari wa Wanyama wa Halmashauri hiyo, alisema kati ya ng’ombe 10,000 waliolengwa, wengi wao tayari wamechanjwa na kutambuliwa kupitia mfumo mpya wa utambuzi wa mifugo.
Wafugaji mkoani humo wamepongeza juhudi za serikali, wakisema kampeni hiyo itaboresha afya ya mifugo na kuongeza uzalishaji.
Gwamaka Mwakang’ata, mfugaji kutoka Kata ya Changarawe, alisema chanjo hizo zitasaidia kupunguza vifo vya mifugo na kuongeza kipato cha wafugaji.
“Tunamshukuru serikali kwa kugharamia chanjo hizi. Zimeleta faraja kwa wafugaji na tija katika uzalishaji,” alisema Mwakang’ata.
Naye Michael Nyalusi kutoka mtaa wa Ngome alisema kampeni hiyo imepunguza kwa kiwango kikubwa magonjwa ya mifugo yaliyokuwa yakiwaathiri wafugaji kwa muda mrefu.
“Hali imebadilika sana. Zamani tulipoteza mifugo mingi kutokana na magonjwa yanayozuilika, lakini sasa tumeona matokeo chanya,” alisema.
________________________________________

IRINGA KUTOA CHANJO KWA NG’OMBE ZAIDI YA LAKI NNE KATIKA KAMPENI YA TAIFA YA CHANJO YA MIFUGO

Поделиться в:

Доступные форматы для скачивания:

Скачать видео mp4

  • Информация по загрузке:

Скачать аудио mp3

Похожие видео

Waziri waKilimo Akabidhi Ng’ombe 36 kwa Wafugaji wa Kaskazini Unguja

Waziri waKilimo Akabidhi Ng’ombe 36 kwa Wafugaji wa Kaskazini Unguja

MIFUGO TABORA YACHUKULIWA SAMPULI

MIFUGO TABORA YACHUKULIWA SAMPULI

TRINITY MEAT PACKERS MASANAFU

TRINITY MEAT PACKERS MASANAFU

I'm Building a Free Pallet House in 129 Days in the Forest

I'm Building a Free Pallet House in 129 Days in the Forest

Shughuli za kiuchumi katika mji mdogo wa  Ilula Iringa.

Shughuli za kiuchumi katika mji mdogo wa Ilula Iringa.

5 ежедневных привычек, которые защищают простату после 60 лет

5 ежедневных привычек, которые защищают простату после 60 лет

Mtia Nia Jimbo la Isimani Apongeza Mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita

Mtia Nia Jimbo la Isimani Apongeza Mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita

Wazee Wa Mila  Wapigwa Msasa Juu Ya Hadhari Ya Rushwa Wakati Wa Uchaguzi

Wazee Wa Mila Wapigwa Msasa Juu Ya Hadhari Ya Rushwa Wakati Wa Uchaguzi

Podcast #195 - Cafeicultura: Desafios e oportunidades

Podcast #195 - Cafeicultura: Desafios e oportunidades

SADIKI WA IRINGA AJINYONGA KISA MADENI, MZAZI MWENZAKE AELEZA

SADIKI WA IRINGA AJINYONGA KISA MADENI, MZAZI MWENZAKE AELEZA "ALINITAFUTA NIMSAIDIE SIKUMSIKILIZA"

СТРАШНАЯ АВАРИЯ! Байконур РУХНУЛ — ЭТО КОНЕЦ? Специальный репортаж

СТРАШНАЯ АВАРИЯ! Байконур РУХНУЛ — ЭТО КОНЕЦ? Специальный репортаж

Whole Goose Feast in the Mountains: Honey, Fruit & Fire Cooking

Whole Goose Feast in the Mountains: Honey, Fruit & Fire Cooking

MAKALA MAALUMU KUHUSU UTIAJI SAINI WA UJENZI WA BARABARA YA IRINGA - MSEMBE (RUAHA NATIONAL PARK)

MAKALA MAALUMU KUHUSU UTIAJI SAINI WA UJENZI WA BARABARA YA IRINGA - MSEMBE (RUAHA NATIONAL PARK)

РОССИЯ: Я исследую САНКТ-ПЕТЕРБУРГ и получаю ПОДАРОК от солдата, который возвращается с фронта

РОССИЯ: Я исследую САНКТ-ПЕТЕРБУРГ и получаю ПОДАРОК от солдата, который возвращается с фронта

How to look after calves for prevention of Mortality rates.

How to look after calves for prevention of Mortality rates.

Хватит выбрасывать старые зажигалки! Как сделать супермощную и долговечную зажигалку

Хватит выбрасывать старые зажигалки! Как сделать супермощную и долговечную зажигалку

NGAJILO NA LIKOTIKO WAFUNGUKA, WAHAHIDI KUINUA UCHUMI WA WANANCHI IRINGA MJINI

NGAJILO NA LIKOTIKO WAFUNGUKA, WAHAHIDI KUINUA UCHUMI WA WANANCHI IRINGA MJINI

ПОСЕДЕЛ за одну ночь в 14 лет. Что немой мальчик ВИДЕЛ в тайге

ПОСЕДЕЛ за одну ночь в 14 лет. Что немой мальчик ВИДЕЛ в тайге

Редкие старые двигатели заводятся со звуком, который взорвет вам уши ▶18

Редкие старые двигатели заводятся со звуком, который взорвет вам уши ▶18

© 2025 dtub. Все права защищены.



  • Контакты
  • О нас
  • Политика конфиденциальности



Контакты для правообладателей: [email protected]