Melodies Of Hope-Ufunuo wa Matumaini
Автор: BMG ONLINE TV
Загружено: 2018-05-17
Просмотров: 125215
Na Imani Hezron, Adventist
Mkutano wa Ufunuo wa Matumaini unaendelea katika uwanja wa CCM Kirumba Jijini Mwanza ambapo mafundisho ya Afya, Kaya, Familia na neno la Mungu yanafundishwa. Muhubiri Mkuu kwenye mkutano huo ulioanza Mei 12, 2018 ni Mchungaji Dkt.Mark Finley kutoka Marekani.
Mkutano huo unaanza kila siku kuanzia saa 16:00 alasiri hadi saa 20:00 usiku huku pia yakikujia mubashara kupitia Hope Chanel Tanzania kwenye visimbuzi vya Continental pamoja na Ting bila kusahau kwenye Youtube. Pia yanapatikana 102.1 Morning Star Radio Mwanza na kwenye programu tumishi (Application) za Itune na TAMC.
Kupitia BMG, Karibu kusikiliza wimbo maalumu wa mkutano huo kutoka kwa vijana wa Melodies of Hope.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: