TANZANIA YAANZA UZALISHAJI WA VIPURI VYA MIGODI NA VIWANDANI
Автор: MOHAB TV ONLINE
Загружено: 2024-09-28
Просмотров: 302
Tanzania imepiga hatua kubwa katika sekta ya uzalishaji wa vipuri vya migodini na viwandani, baada ya Kiwanda cha kisasa cha East Africa Conveyor Supplies Limited (EACS) kilichopo Kahama, Shinyanga kuanza rasmi uzalishaji wa vipuri vya mitambo vinavyotumika kwenye migodi na viwanda mbalimbali ndani na nje ya nchi, ikiwa ni matokeo ya jitihada za Serikali katika kuweka mazingira bora na wezeshi ya uwekezaji hapa nchini pamoja na Ushiriki wa Watanzania katika Sekta ya Madini.
Akizungumza Mjini Kahama, Mkoani Shinyanga na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Madini, Mkurugenzi Mtendaji wa EACS, Peter Kumalilwa, alisema kuwa kiwanda hicho kinachomilikiwa kwa ubia wa asilimia 50 Mtanzania na asilimia 50 Wageni kimeanza uzalishaji mwezi Mei 2023, ambako hivisasa vipuri vinavyozalishwa ni pamoja na steel conveyor frames, drop brackets, steel conveyor rollers, impact conveyor rollers, plastic na steel caps for conveyor rollers na bidhaa hizo zinauzwa kwenye migodi mbalimbali nchini Tanzania kama Barrick North Mara, Barrick Bulyanhulu na Buckreef, pamoja na migodi iliyo katika nchi jirani kama Kibali Gold Mine uliopo Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Lumwana Mine uliopo nchini Zambia.
KITUO KINACHO JIHUSISHA NA HABARI MBALIMBALI ZA KIJAMII NA KUELIMISHA UMMA KUHUSU MATUKIO YANAYO JIRI KILA WAKATI HAKIKISHA UNA SUBSCRIBE CHANEL YETU USIPITWE NA TUKIO LOLOTE HAPA NCHINI ( Email: [email protected](+255752268249 / +255785537878)
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: