OPERESHENI KALI YA UKAGUZI WA VYOMBO VYA MOTO - MWANYANYA
Автор: ASAM Online TV
Загружено: 2025-12-18
Просмотров: 8557
Katika kuhakikisha wamiliki na waendesha vyombo vya moto wanatii sheria zilizowekwa ikiwemo ulipaji wa tozo zinazotakiwa, Mamlaka ya Usafiri na Usalama Barabarani kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wamefanya operesheni maalum ya kukagua vyombo vya moto vinavyotoa huduma za kusafirisha wananchi katika eneo la Mwanyanya, Mkoa wa Mjini Magharibi.
Akizungumza kuhusu operesheni hiyo, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri na Usalama Barabarani, Ndg. Haji Ali Zubeir, amesema wamebaini uwepo wa vyombo vingi vinavyotoa huduma hizo vikiwa na madeni pamoja na kutokupasishwa, jambo ambalo ni kosa kisheria.
Aidha, Ndg. Zubeir amewaasa wamiliki wa vyombo vya moto kutii sheria bila ya shuruti kwa kuhakikisha vyombo vyao vinakidhi vigezo vilivyowekwa.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: