MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA ZIMBABWE AWASILI NCHINI KWA MUALIKO WA DKT. MPANGO
Автор: Selphix Media
Загружено: 2025-08-30
Просмотров: 11
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe, Mheshimiwa Kanali (Mst) Kembo Campbell Mohadi amewasili nchini leo tarehe 30 Agosti, 2025 kwa ziara ya kikazi ya siku 2.
Ziara hiyo ipo ndani ya tarehe 30-31 Agosti, 2025 kwa mwaliko wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. @dr_philip_isdor_mpango.
Alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Mhe. Makamu wa Rais Mohadi alipokelewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. @cosatochumi_ na viongozi wengine waandamizi wa Serikali.
Akiwa nchini, Mheshimiwa Makamu Rais Mohadi
atakuwa na mazungumzo rasmi na mwenyeji wake,
Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango Ikulu jijini
Dar es Salaam na baadaye kuzungumza na
waandishi wa habari.
Aidha, Mheshimiwa Mohadi atatembelea Shule ya
Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere iliyopo Kibaha, Chuo cha Kilimo na Mifugo kilichopo Kaole, Bagamoyo na Kituo cha Urithi wa Ukombozi barani Afrika cha jjini Dar es Salaam.
.
.
Endelea kufuatilia @selphix_media kwa Habari Zaidi
#SelphixUpdates #selphix_media
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: