WADAU WA MAMLAKA YA ANGA WAKUTANA TANGA, LENGO NI UTOAJI WA HUDUMA BORA KWA ABIRIA.
Автор: Tanga TV Online
Загружено: 2025-11-18
Просмотров: 312
Mamlaka ya usafiri wa anga nchini imefanya kikao cha tathimini ya huduma wanazotoa katika viwanja vya ndege vyote vya hapa nchini.
Akizungumza wakati wa kufungua kikao cha kamati ya Taifa ya uwezeshaji na urahisishaji wa huduma za anga Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi, Dkt, Batilda Burian amewaomba kutanzama na kufanya haraka katika kuboresha huduma za kiwanja cha ndege cha Tanga na mombo ili kurahisisha huduma za uwekezaji na kukuza utalii katika mkoa huu.
Akielezea mikakati ya Mamlaka ya usafiri wa anga Mkurugenzi mkuu wa mamlaka hiyo Salim Msangi amesema kwa sasa wameanza maboresho katika viwanja vyote nchini lengo ni kutoa huduma bora kwa abiria na kuongeza tija katika usafiri huo.
Pia Mkurugenzi Salim amesema mamlaka na kamati inaendelea kufwatia magonjwa ya milipuko yanayotokea katika nchi za jirani na kudhibiti isiingie katika nchi.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: