WAZIRI MKUU AZINDUA MELI MPYA YA MV NEW MWANZA, ATOA MAAGIZO KWA MIRADI ILIYOSIMAMA
Автор: BONGO PLAY TELEVISION
Загружено: 2026-01-23
Просмотров: 34
Waziri Mkuu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba leo tarehe 23 Januari, 2026 amezindua rasmi meli mpya ya kisasa ya Mv. New Mwanza iliyojengwa na Mkandarasi Gas Entec Ship- Building kutoka Korea kwa gharama ya Tshs. Bilioni 120.56.
Akizungumza na wananchi katika eneo la Bandari ya Mwanza Kusini Mhe. Waziri Mkuu amesema kuwa ujenzi wa Meli hiyo ya kisasa ni ishara ya juhudi za serikali kuwaletea maendeleo wananchi kwa kuhakikisha wanamaliza kiu ya kuwa na usafiri imara katika ziwa Victoria.
Aidha, ameiagiza Wizara ya Uchukuzi kuendeleza ujuzi uliotumika kujenga meli hiyo, TASHICO washirikiane na wadau wengine kulinda mradi huo kwa kuweka bima na kufuata ushauri wa kitaalamu na kuimarisha na kukuza diplomasia ya mahusiano na amani.
Доступные форматы для скачивания:
Скачать видео mp4
-
Информация по загрузке: